Matthew 26:1-6

Shauri Baya La Kumuua Isa

(Marko 14:1-2; Luka 22:1-2; Yohana 11:45-53)

1 aIsa alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake, 2 b“Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”

3 cBasi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa. 4 dWakafanya shauri ili kumkamata Isa kwa siri na kumuua. 5 eLakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”

Isa Anapakwa Mafuta Huko Bethania

(Marko 14:3-9; Yohana 12:1-8)

6 fIsa alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
Copyright information for SwhKC